Tuesday, May 31, 2011

BERRY BLACK NDANI YA COVENTRY JUMAMOSI TAR 04 JUNE,2011

Wednesday, May 25, 2011

LEO TUCHEKE KIDOGO...

                                                                   chanzo:orijino komedi

20% - Tamaa Mbaya

Tuesday, May 24, 2011

FACEBOOK KIBONGO BONGO..

Mimi nimejiunga facebook ili kukutana na marafiki niliopotezana nao muda mrefu mfano Classmates,School mates, University mates,Work/field mates na wengine ili kujuliana hali (kuwasilina kama marafiki), kudumisha  urafiki na kupashana habari zinazo tokea kila mtu alipo kwa wakati ule.Facebook inasaidia kupata marafiki mlipotezana nao hata marafiki wapya na kuwakutanisha

                                                           Facebook logo

Facebook inasaidia kukutanisha watu kwa matukio mbalimbali ya kijamii mfano weddings,parties,kucheza games mbalimbali,kutangaza biashara; kisiasa mfano: mikutano,maandamano; kisayansi mfano: kuendesha mijadala ya kitaaluma na mambo ya teknolojia i.e IT,.Huko Egypt (Misri) Facebook imesaidia kukutanisha watu ambao wameweza hata kuing'oa serikali ya  muda mrefu ya Hosni Mubarak  (14 October 1981 – 11 February 2011) na hata watoto kubatizwa 'Facebook' kama kumbukumbu ya tukio hilo.

Watanzania wengi tumejiunga Facebook kwa kasi kubwa tu,ni vizuri japo sijajua kama matumizi ya huu mtandao yapo sawa! Kwa mtumiaji wa facebook unaweza kua unanielewa.Wengine picha tunazoweka humo ni utata mtupu mfano mtu kaweka picha ya makalio yake tu yakiwa tupu ama nguo inayo onyesha maungo,shanga kiunoni,lips peke yake,au mwili wote ukiwa  na chupi tu,kifua wazi ili iweje? au mtu kaweka picha yenye maneno 'I've the p**sy (ni tusi siwezi andika lote)  so I make the rules' ili iweje?.

Tujiulize tumejiunga facebook ili iweje?.Mtu unakuta yupo ofisini the whole day yuko online (sio idle)  facebook hio kazi anafanya saa ngapi? Mimi nimeona facebook kwa bongo ni 'more of a dating site' je wewe unaionaje? au unaichukuliaje?.Kiufupi madhara ya facebook ni makubwa kuliko, mfano watu wengi wamefukuzwa kazi,ndoa nyingi zimevunjika,watu wengi wameuawa kwa kupitia facebook hasa wale wasio ogopa kukutana mtu usiye mjua,kubakwa,kufungwa, mahusiano mengi yamevunjwa,na watu wengi  sasahivi hufuta (deactivate) akaunti facebook wanapooa,kuolewa ama kugonganisha wapenzi.Be careful na facebook kabla huja umbuka...na pia nijibu......

                                        Wewe umejiunga facebook ili iweje?
                                      Kiraka amejiunga facebook ili......

                                     Ochu anajibu hilo swali msikilize hapa chini




UFUNGUKAJI WA WASANII WETU OVYO!!

Hapa chini ni video ya Clouds Tv 'Take one' 'MTU KATI' na Zamaradi.Angalia vizuri hii Video clip then sikiliza mtu kama msanii ambaye ni kioo cha jamii anapo ongea katika chombo cha habari.Kuna kipengele anasema usanii wake umemuweka karibu na mabinti,imempa mademu,imemuongezea upendo kwa mademu!!! huyu ndio kioo cha jamii!! ...Ninge elewa angesema usanii wake umemuweka karibu na watu SIO MADEMU (HII NI PUMBA).Pia anasema hua anafanya ukauzu kwa mademu wanao mtega kwa kuvaa miwani tinted kwa maana hio ''katufanyia ukauzu Watanzania tunao angalia hii interview kwa kutuvalia hio miwani'' MAELEZO YAKE HAYAJA JITOSHELEZA!!

Si kwamba na 'hate' kwanza simfahamu namsikia tu....Kiukweli ameongea kituko cha mwaka coz movie hawangalii mademu peke yao,aidha kwenye hii interview MNYONGE MNYONGENI HAKI YAKE MPENI.. nimependa kipengele cha matumizi mabaya ya lugha katika movie zetu (movie editors kama wapo wawe makini na kazi yao) na sehemu nyingine zote uozo mtupu na ameaibisha wasanii wenzie (mtazamo wangu)...sikiliza halafu nipe mtazamo wako pia (ni mtazamo tu)

Msikilize Hemed akifunguka hapa chini (Aibu)
(kwa hisani ya Zamaradi Mketema)
                                                         

Vituko vingine vya wasanii angalia hapa: http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/hasheem-thabeet-afanya

Monday, May 23, 2011

SIMBA SC KUVAANA NA BIRMINGHAM CITY FC JULY 7 MWAKA HUU

Timu ya mpira Simba Sports Club ya Dar es salaam kuvaana na Birmingham City Football Club ya Uingereza Julai 7,2011.Hayo yatategemea kuthibitishwa baada ya timu ya wataalamu toka Uingereza kuona kiwango cha uwanja na mazingira kiujumla kimichezo baada ya kukagua tarehe 16/05/2011.Kama mechi hio itaridhiwa Birmingham City ita ambatana na mashabiki  wasio pungua 1000 watakao jilipia gharama za safari na malazi wenyewe wakati timu itajipatia vijisenti visivyo pungua Dola Million 1.2 na kulala hotel nzuri.

                                kikosi cha timu ya simba

Mpaka sasa safari ya BCFC kwenda Tanzania haijathibitishwa baada ya ukaguzi ulio pangwa ufanywe tarehe tajwa hapo juu na pia kutokana na ratiba za mechi za hapa ulaya.Baada ya hayo yote kukamilika ndipo safari itathibitishwa.Pia nimetembelea mtandao wa Simba SC (http://simbasportsclub.co.tz/v3/)  hakuna taarifa yoyote kuhusu mechi hio sasa sijajua mashabaki tutajua nini kinaendelea maana menu zenyewe hazina maelezo yoyote yaani hata menu iko empty: Mfano events,matches,News hakuna kitu-sijui labda nimeingia sio site yenyewe kuna anayejua anipe site halisi please! maana kama ndio yenyewe bado hatupo siriazi kiukweli maana haina cha maana zaidi ya orodha ya viongozi,wachezaji na historia ya timu!!!!!.Angalieni Yanga http://www.yangasc.com/

Anyways, hongereni Simba kama hio mechi itachezwa na nawatakieni ushindi dhidi ya wazungu!.

soma zaidi hapa:http://www.goal.com/en/news/89/africa/2011/05/03/2469421/birmingham-city-officials-to-inspect-facilities-in-tanzania
                          : http://www.birminghampost.net/midlands-birmingham-sport/west-midlands-sports/birmingham-city-fc/2011/04/18/birmingham-city-tanzania-confirmed-as-potential-destination-for-pre-season-tour-97319-28542251/

LIMO YA OBAMA MAARUFU KAMA ''BEAST'' YABUMA ZIARANI IRELAND

Gari moja wapo katika msafara wa Obama  huko Ireland yabuma baada ya kugonga tuta nje ya ubalozi wa Marekani jijini Dublin-Ireland.Gari hilo aina ya Cadillac la Mr Obama lenye jina maarufu kama ''The Beast'' Yaani 'Mnyama' kwa kimakonde lilisekana kubeba wataalamu wa ulinzi katika msafara huo wakati Rais wa Marekani Barack Obama akiwa ziarani nchini humo jana tarehe 23/05/2011.

Umati mkubwa wa watu umeshuhudia tukio hilo 'live' ambapo mlio mkubwa ulitokea baada ya chesis lake kugusa tuta na kushindwa kwenda mbele na muda si mrefu waliletewa gari lingine kuendelea na msafara.


Kama uonavyo kwenye video hapo juu hicho ndicho kilichotokea.Limo/The Beast hilo lina  urefu wa futi 18 na uzito wa tani 8 na upana wa chuma cha bodi wa inch 8 halipitishi bomu wala risasi na lina lina oxygen yake ndani.Rais Obama akiwa ndani ya hilo gari nick name yake inakua Cadillac one na sio The Beast.  The beast inasemekana kua na camera kila kona,shotguns na vingine vingi kwa ulinzi zaidi                               


Mafundi wakinasua The Beast iliponasa



The Beast katika mchoro

(chanzo:dailymail)





                                                                                                                                                                            

UNAIKUMBUKA HII??

Hiki kiatu kilikua maarufu sana zamani siku hizi sikioni tena sijui bado kinavaliwa? Na kama kinavaliwa sijui utaanguka mara ngapi kwenye hizi barabara zetu? Hiki huvaliwa na suruali yake (hasa draft) ambayo ni pana kwa chini nyembamba karibia kubana fulani kwenye magoti.Si kila mtu alikua na kiatu kama hiki jina kama sikosei ni Laison (kama kuna jina lingine usisite nitafurahi kulijua). Pia sikumbuki ni miaka gani ila zamani niliweza ona watu wachache wanavaa na ilikua fashion by then.Wewe je umewahi kuona hiki kiatu? je kina kukumbusha nini??

Friday, May 20, 2011

ATI UMASIKINI WA TANZANIA NI LAANA???

Hebu sikiliza mjadala huo hapo chini na useme mtazamo wako kama ni laana au tunajitakia kua masikini? je  kila mmoja wetu katika jamii tunayo ishi anawajibika kwa nafasi yake au ndio tunanyoosheana vidole kuonyesha  kijibanzi kwenye jicho la jirani wakati sisi tuna boriti machoni mwetu? Penye wengi hapa haribiki neno, maswali ni mengi ila kwa sasa tuangalie haya kwanza kama ni laana,tunajitakia,hatuwajibiki,hatuja wezeshwa,uzembe,bora liende,aliye shiba hamjui mwenye njaa au ndio niseme kama wanavyosema kwetu kule ''TUNGAYA SIDA'' YAANI HATUNA SHIDA KABISAA YAANI YOTE SAWA TU?? SEMA USIKIKE!!!

SEHEMU YA KWANZA


SEHEMU YA PILI


CHANZO:MWANAKIJIJI




Thursday, May 19, 2011

DOLLAR MILLION 6 ZAMUOKOA

Hatimaye aliyekua Mkurugenzi wa IMF  Dominique Strauss-khan akubaliwa kutoka rumande kwa dhamana ya Dollar Million 6 ( $6m) na masharti makali ikiwemo kua chini ya ulinzi kutoka kampuni binafsi kwa gharama ya Dollar laki mbili kwa mwezi ambazo ni juu yake,kuwekwa chombo cha kisasa mguuni kitakacho onyesha alipo kwa saa 24 kila siku,kufungwa kwa video camera katika nyumba atakayo kaa na alarms kumzuia asitoke.

Mheshimiwa huyo ambaye mpaka sasa amejihudhuru wadhifa wake kama Mkurugenzi wa IMF kwa takribani miaka minne kutokana na kashfa ya kutaka kubaka mhudumu wa hotel huko Marekani,ataachiwa na kwenda kuishi kwa muda katika nyumba ya muda ambako mkewe Heiress, Anne Sinclair, mwanahabari na  Millionea wa kifaransa amempangishia wakati akisubiri kesi yake kusikilizwa hivi karibuni.
Zaidi soma hapa kwa kiingereza: http://www.dailymail.co.uk/news/article-1388834/Wife-daughter-disgraced-IMF-boss-arrive-court-appeal-bail-hearing.html#ixzz1MrCCmdJV

IKO WAPI HII??!

VIJISENTI VINAPOSHINDWA KUKUSAIDIA..

Mkurugenzi mkuu wa shirika la fedha duniani (IMF) bwana Dominique Strauss-Kahn ambaye pia ni mwanasheria,mwanasiasa na mwanauchumi wa kifaransa amewekwa jela Marekani kufuatia madai ya kutaka kumbaka mhudumu wa Hotel (Hotel Maid).Baada ya kukamatwa na kufikishwa mahakamani kufuatia kitendo hicho bwana Strauss-Kahn kupitia mwanasheria wake aliomba aachiwe kwa dhamana ya (vijisenti)  Dollar Million moja ($1m) mahakama ilikataa dhamana hio na kumrudisha rumande.


                                       Aliyekua mkurugenzi wa IMF-Dominique Strauss-kahn 

Kufuatia skendo hio mkuu huyo wa IMF amelazimika kujiuzulu wadhifa wake ambapo Umoja wa nchi za Ulaya (EU) wamesha tangaza kinyang'anyiro na wagombea wa awali ni kama ifuatavyo:-

  • Mohamed El-Erian, Egypt

  • Stanley Fischer, Israel

  • Gordon Brown, UK

  • Kemal Dervis, Turkey

  • Peer Steinbrueck, Germany

  • Montek Singh Ahluwalia, India

  • Christine Lagarde, France

  • Agustin Carstens, Mexico

  • Trevor Manuel, South Africa

  • Axel Weber, Germany
  • ETI JUMAMOSI TAREHE 21/05/2011 MWISHO WA DUNIA???!!

    Imeripotiwa kutokea wahubiri wa kidini jijini New York-Marekani kufuatia wanacho dai mwisho wa dunia ni tarehe 21/05/2011 ambayo ni siku ya Jumamosi.Wahubiri hao ambao wamekua wakifanya kazi hio bila kuchoka wametoa vielelezo mbali mbali kuthibitisha tukio hilo.Zaidi wamedai tukio hilo si lazima litokee wakati mmoja duniani kote kufuatia kutofautiana masaa lakini lazima iwe tarehe iliyo tajwa!!

    Ni matumaini yangu hayata tokea yale ya Kibwetere wa Uganda kuchoma moto waumini wake wanao sadikika  kufika 1000 ndani ya kanisa la '' Amri kumi za Mungu'' eti mwisho wa dunia umefika na kubaki yeye na bosi msaidizi wake  Bi Credonia Mwerinde nje mnamo Machi 17 mwaka 2000.Hata hivyo mpaka sasa haijulikani kama Kibwetere  na mwenzie wapo hai na polisi wa Uganda kwa kushirikiana na wale wa kimataifa (Interpol) bado wana mtafuta Kibwetere popote alipo Duniani. Pamoja na kua na maswali mia nane kidogo mie yangu macho!!

    Kwa habari zaidi soma hapa:http://uk.news.yahoo.com/preachers-prophesying-end-world-york-000338169.html

    Zaidi kuhusu Kibwetere soma hapa:http://www.culteducation.com/kibwetere.html

    Tuesday, May 17, 2011

    50 CENT IS BACK, ANAKWAMBIA ''DIAL 911''

          NB:****SONG CONTAIN STRONG LANGUAGE,PLEASE BE WARNED****






    MAMBO YA KIPANYA...

    Sasa kama hali ndio hii uhuru wa vyombo vya habari uko wapi?






    IPI NI SAHIHI?

    HII?

                                                              AU HII HAPA CHINI


                                                                               AU HII

    Sunday, May 15, 2011

    BAFANA BAFANA 1 TAIFA STARS 0

    Timu ya Taifa ya Africa kusini maarufu kama Bafana Bafana au Boys Boys or Go Boys Go Boys jana Jumamosi ya tarehe 14/05/2011 imeibanjua Taifa Stars ya Tanzania 1-0 kwenye mechi ya kirafiki iliyofanyika uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam.Bafana Bafana ilijipatia goli lake hilo kipindi cha kwanza kupitia mchezaji wake Siyabonga Sangweni (29) jezi namba 44.Hilo ndo lilikua gori pekee lililo ipa Bafana Bafana ushindi mpaka mwisho wa mchezo

    Man of the match Siyabonga Sangweni

    Habari zaidi za mechi hio bonyeza link:
    http://supersport.com/football/bafana/news/110514/Bafana_defeat_Taifa_Stars

    Tuesday, May 10, 2011

    Kila Mmoja- Nonini ft Lady Bee & Chege TMK

    Sunday, May 8, 2011

    DUNIA IMEKWISHA......

    YAANI NIMETAMANI KUJIFICHA BAADA YA KUONA HII KITU KUCHEKA IMESHINDIKANA NA SINA CHA KUONGEA ZAIDI HAPA SEE FOR YOURSELF....

    SOURCE:NTV

    Saturday, May 7, 2011

    SHAME ON YOU SCAMMERS!!!!!!!!!

           ''Can I Give You This Trust?....NO THANK YOU!!...   Reply Immediately.(ILI UIBIWE HARAKA LOL)

    Dear Friend,
    I am ( Mr.David Chalimo )The Head of files/Recording Department in a bank Burkina Faso in African.I Hoped that you will not expose or betray this trust and confident that i am about to repose on you for the mutual benefit of our both families.I need your urgent assistance in transferring the sum of $ 15 million U.S dollars ( fifteen million U.S dollars) into your account.

    The money has been dormant for yearas in our Bank here without any body coming for it.I want to release the money to you as the nearest person to our deceased customer(the owner of the account)who died a long witah his supposed next of kin in an air crash few years ago.I don't want the money to go into our Bank treasury account as unclaimed fund. So this is the reason why i contacted you, so that we will release the money to you as the nearest person to the deceased customer.

    Please I would like you to keep this proposal as a top secret or delete it from your mail box ,if you are not interested.Upon receipt of your reply,I will send you full details on how the business will be executed and a text of application which you will fill and send to the bank for the release of the money to your account.Also note that you will have 40% of the above mentioned sum, if you agree to transact the business with me while 60% will be for me.

    I will not fail to bring to your notice that risk is free in this transaction and that you should not entertain any atom of fear as all required arrangements have been made for the transfer.Please for full trust,don't forget to reply with your contact information like-:Your Name,Age,Marital Status.,Cell Phone
    Number,Your Country,Your House Address,Your Occupation,Sex,Religion,Your ID Card Or International Passport and Your Private E-mail Address for full trust.

    Looking forward to haear from you immediately
    Mr.David Chalimo




    Friday, May 6, 2011

    JOSE MOURINHO APEWA BAN YA MECHI TANO

    Jose Mourinho (Meneja Real Mdrid)
    Meneja wa timu ya Real Madrid Jose Mourinho apewa ban ya mechi tano ikiwa ni adhabu kutoka UEFA kufuatia kushangilia kinafiki baada ya kutolewa uwanjani mchezaji wa Real Madrid 'Pepe'  na baadae Wolfgang Stark  mwamuzi katika mechi hio  kali baina ya Barcelona na Real Madrid kumpa kadi nyekundu Jose ambaye alionekana kushangilia adhabu ya mchezaji wake.

    Adhabu hio ni sambamba na faini ya Euro 50,000  kwa Jose Mourinho na 20,000 Euros kwa kilabu hicho kufuatia utovu wa nidhamu wa washangiliaji wa Real Madrid uwanjani siku hio ya mchezo ambapo Barcelona waliibuka kidedea kwa 2-0 usiku huo dhidi ya Real Madrid.Pepe mwenyewepia alipewa ban ya mechi moja na kwa upande wa boss wake (Mourinho) amesha tumikia adhabu hio kwa kuto hudhuria mechi moja na kilabu hicho kimedai kukata rufaa kwa adhabu  zilizo tolewa mapema iwezekanavyo.

    zaidi soma hapa: http://www.skysports.com/story/0,,11833_6916716,00.html

    AL-QAEDA WATHIBITISHA KUUWAWA KWA OSAMA

    Habari zilizo jiri hivi karibuni toka kundi la kigaidi la Al-Qaeda ni kwamba kiongozi wao Osama Bin Laden ni kweli ameuawa na Marekani nchini Pakistan eneo la Abbottabad.Habari hizo zimenaswa kwenye mtandao unaosadikika kutumiwa  na kundi hilo wakidai shangwe za Marekani kwa kifo cha kiongozi wao kitageuka kua huzuni hivi karibuni.Hata hivyo kundi hilo limeahidi kuwepo kwa mashambulizi mapya kwa Marekani na washirika wake kusherekea miaka kumi ya mauaji ya 9/11 Marekani.Hio ni sambamba na kuishinikiza Pakistan kuandamana kwa kitendo cha Marekani kumuua Osama.


    Katika upande mwingine Marekani imedai shambulizi la kumuua Osama limewawezesha kupata habari ambayo Osama ali rekodi siku chache baada ya kifo chake.Habari hio ilikua ni ya mashambulizi ya kulipua Reli na treni huko Marekani.


    Kwa habari zaidi soma hapa: http://uk.news.yahoo.com/bin-laden-plotted-attack-us-trains-022222947.html


           na hapa                                  : http://news.sky.com/skynews/Home/World-News/Video---Osama-Bin-Laden-Barack-Obama-At-Ground-Zero-Amid-Pakistan-Compound-Raid-Story-Doubts/Article/201105115986145?lpos=World_News_Third_Home_Page_Article_Teaser_Region__4&lid=ARTICLE_15986145_Video_-_Osama_Bin_Laden%3A_Barack_Obama_At_Ground_Zero_Amid_Pakistan_Compound_Raid_Story_Doubts

    Tuesday, May 3, 2011

    ATI NINI??

    NANI ALAUMIWE??

    Hivi mwanafunzi kama huyu akifeli ata mlaumu nani?. kweli walimu wetu wana kazi kubwa sana kama mambo yenyewe ndio haya.Hivi kwani mtu huwezi zima simu ukiwa darasani ok, kuzima ngumu weka silent basi kwani simu kuita darasani mbali na kukupotezea muelekeo katika kipindi inaharibu utulivu na mwendelezo wa kipindi darasani.Mie naona wanafunzi wa aina  hii aidha wanyang'anywe simu kama hawaweza fata masharti au watolewe nje ya darasa waka ongee vizuri huko nje kama simu ina umuhimu kuliko kipindi.

    Maadili Mashuleni (Kazi safi ya Haki Elimu)


    Ni wazi kwamba serikali haiwezi kufanya kila kitu kudhibiti maadili ya wanafunzi ila inawezekana kwa ushirikiano wa wazazi, walimu ama walezi.Kwa wazazi kama unamnunulia mtoto wako simu ni vema umwambie matumizi ya hio simu akiwa shule, kwa walimu ni vema kuwaambia au kuweka tangazo linalo zuia matumizi ya simu muda wa masomo au darasani.Pia wazazi tuwe karibu na watoto wetu kujua hata wanaishi vipi na shule wanaendeleaje,utakuta mtoto ana simu ambayo hata baba au mama hawana (nina maana ya Gharama sana) mnunuzi hajulikani na simu hio hutumika wakati wa shule na usiku nyumbani wakati hata wazazi hio namba hawaijui.

    Kama wazazi tunajiweka mbali na watoto wetu wa shule basi hata wasipo faulu tusilalamike.Ijulikane kwamba kusoma inahitaji moyo na faraja ya wazazi ni muhimu katika masomo.Ni lazima mzazi ujue maendeleo ya mwanao angalau kwa kila muhula.Kwakuto fatilia maendeleo ya mwanafunzi ndio siku ya siku unakuta mtoto wako ni mvuta bangi tu shule inamboa haitaki tena, kafukuzwa ana mimba (kwa wasichana) au tu amekua mtoto aliyekosa maadili kwa namna zote.Zamani mtu anaweza sema hajui sasa haki elimu ndio hao wanafichua maovu mashuleni.Wazazi,Waalimu pamoja na Serikali ni lazima tuwajibike sehemu zinazo tuhusu.

    SICK TUNES ONCE AGAIN

    WARNING:Be advised that some songs in this list (hereunder) contain strong language!! i'm warning you!.

                                                          Auburn-la la la

    Iyaz- island girls
                                                                      
                                                                      Jeremiah ft 50 Cent-down on me

                                                             Chris Brown-Beautiful people
                                      
                                           YC ft Racks-future

    Wiz Khalifa-this plane

     Waka Flocka- No Hands

    NELLY-Just a dream

    N Dubz-Girls (clean version)

    Enrique Iglesias - One Day At A Time (feat. Akon) 

    Monday, May 2, 2011

    BREAKING NEWS:OSAMA BIN LADEN IS NO MORE!!


                                                    Osama  Bin Laden enzi za uhai wake.

    Kiongozi namba moja wa kundi la kigaidi la Al-Qaeda (pichani juu) Osama Bin Laden ameripotiwa kuuwawa na majeshi ya Marekani nchini Pakistan baada ya mapigano makali ya kurushiana risasi kabla ya kifo chake.Habari zilizo tapakaa mitandaoni zinathibitisha kifo cha Osama ikiwa ni baada ya taarifa ya ikulu ya Marekani kuthibitisha kifo hicho kupitia hotuba ya Rais wa Marekani, Barack Obama ambaye amekaririwa akisema''to those families who have lost loved ones to Al-Qaeda's terror justice has been done''

    Osama wakati akitafutwa kwa dili la dola million moja kwa atakaye mpata

    Hata hivyo Rais Obama ame tahadharisha balozi zake zote duniani kuwa makini kwa sasa kwani kuna uwezekano wa washirika wa Osama kulipiza kisasi kufuatia kifo cha kiongozi wao. Osama amekua akitafutwa na Marekani kwa muda sasa kufuatia shambulizi la Sept 11,2001 huko New York na Washington ambapo watu karibia 3000 walipoteza maisha.Huko Marekani watu leo wanasherekea kifo cha Bin Laden kwa shangwe zote.Watu mbali mbali pia wamesema Al-Qaeda sio Osama pekee (lile ni kundi kubwa sana) kwahio kazi haijaisha.

    Zaidi soma hapa:http://www.bbc.co.uk/news/world-us-canada-13256676
                               :http://latimesblogs.latimes.com/washington/2011/05/osama-bin-laden-dead-al-qaeda-islamabad-navy-seals.html
                               : http://www.guardian.co.uk/world/2011/may/02/osama-bin-laden-arab-reaction
                               :http://www.msnbc.msn.com/id/42852700/ns/world_news-south_and_central_asia/